CLOUD: NITAMSHUSHIA ZA CHEMBE JB
MWIGIZAJI na prodyuza wa filamu Bongo, Issa Musa ‘Cloud 112’ amefunguka kuwa atamtandika ngumi kali za chembe mpinzani wake, Jacob Steven ‘JB’ katika pambano litakalopigwa kesho kwenye Tamasha la Matumaini, Uwanja wa Taifa, Dar.
Mwigizaji na prodyuza wa filamu Bongo, Issa Musa ‘Cloud 112’
Akipiga stori na Amani mara baada ya…
MWIGIZAJI na prodyuza wa filamu Bongo, Issa Musa ‘Cloud 112’ amefunguka kuwa atamtandika ngumi kali za chembe mpinzani wake, Jacob Steven ‘JB’ katika pambano litakalopigwa kesho kwenye Tamasha la Matumaini, Uwanja wa Taifa, Dar.
Mwigizaji na prodyuza wa filamu Bongo, Issa Musa ‘Cloud 112’
Akipiga stori na Amani mara baada ya kusikia JB akijitapa kwenye mitandao ya kijamii kuwa atamshushia ngumi 12 katika raundi ya kwanza, Cloud 112 alisema kitu hicho hakitatokea na badala yake atamtandika yeye.
Jacob Steven ‘JB’
“JB hana uwezo wa kunipiga mimi, anaanzaje kwanza! Nitampiga ngumi kali pale taifa hadi hasinisahau, asicheze na mimi kabisa, namba nyingine hii,” alisema Cloud.
Mbali na mpambano huo, tamasha hilo linatarajiwa kupambwa na matukio mengi ya kusisimua ikiwemo burudani ya wanamuziki wa Gospo na mechi za wabunge wa Simba na Yanga.
Comments
Post a Comment